Ndagoni Pemba kuchagua Diwani mpya Febuari 18 mwakani.

Tume ya uchaguzi Zanzibar imetowa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusiana na uchaguzi mdogo wa wadi ya ndagoni kufuatia kufariki kwa diwani wa wadi hiyo.
 
Akizungumza na wandishi wa habari mkurungezi wa tume ya uchaguzi Zanzibar Salum  kassim Ali amesema kuwa uchaguzi huo mdogo utafanyika kufuatia kufariki kwa aliyekuwa diwani wa Ndagoni  Juma Ali Kombo .
 
Amesema kuwa uchaguzi huo unatarajia kufanyika tarehe 18 february 2017. 
Pia amewataka wananchi wa ndagoni kujitokeza kupiga kura itakapofika  Tarehe 18 february 2017 kwa ajili ya kumchaguwa diwani wa wadi hiyo.
 
chanzo;ZANZIBAR 24

Comments