Hukumu
hiyo imetolewa na hakimu wa mahakama hiyo, Ahmed Jumbe Marika chini ya
kifungu 311 sheria namba 7 ya mwaka 2004, kutokana na kuwa mshitakiwa
namba mbili Hassan Khamis Rashid (18), anakabiliwa na kosa kama hilo, na
yupo jela anatumikiwa kifungo cha mwaka mmoja na miezi sita.
“Kutokana
na madai ya upande wa mashitaka kuwa mshitakiwa namba mbili, anatumikia
chuo cha mafunzo, hivyo mahakama imewapunguzia adhabu chini ya kifungu
311 sheria namba 7 ya mwaka 2004 wote kwa pamoja kutumikia kifungo cha
mwaka mmoja badala ya miaka mitatu.
Akisoma
shitaka hilo, mwendesha mashitaka wa mahakamahiyo Mohamed Ali Juma
alisema mbele ya washitakiwa hao kuwa shitaka lao lipo kwa ajili ya
hukumu ingawa wenzao wawili hawakufika mahakamani bila ya taarifa
zozote.
“Muheshimiwa
hakimu shitaka hili lipo mbele yako kwa jaili ya kutolewa hukumu dhidi
ya washitakiwa, ila kutokana na washitakiwa wawili ambapo ni mshitakiwa
nambari tatu na namba nne hawakufika mahakamani na hakuna sababu za
msingi ama, taarifa zozote ni vyema mahakama ikaangalia kwa kina na
kutoa hukumu inyofaa dhidi yao ili iwe fundisho kwao na wa
wengine,”aliiambia mahakama mwendesha mashitaka huyo.
Washitakiwa
hao Abeid Khamis Abeid (29), Hassan Khamis Rashid (18), Ibrahim Burhan
Yussuf (23) na Mohamed Sharif Mohamed (37) wote kwa pamoja mnamo
Septemba 8 mwaka 2015, majira ya saa 4:15 usiku, Msikiti Kitibegi Wawi
Chake Chake, waliiba Piki piki aina ya Freedom Prima 125 yenye namba ya
usajili 2609 DM yenye thamani ya shilingi 2,220,000 mali ya Said Mohamed
Sadik.
Kosa la Wizi ni kinyume na kifungu 274 (1)cha sheria nambari 6 ya mwka 2004 jambo ambalo ni kosa kisheri
chanz ;zanzibar24.
Comments