Mufti Mkuu wa Zanzibar ameyalaani matamshi yaliotolewa na Abdallah Saleh.

Mufti Mkuu wa Zanzibar Saleh Omar Kaabi ameyalaani matamshi ya kumkashifu Allah (S.W) pamoja na Mtume Muhammad (S.A.W) yaliotolewa na Abdallah Saleh Abdallah.

Amesema kuwa maneno yaliotolewa na kijana huyo ni ya dharau kwa Mwenyezimungu na udhalilishaji kwa mtume Muhammad pamoja na waislamu wote ni maneno ambayo hayawezi kupuuzwa bila ya kuchukuliwa hatuaza kisheria.

Ameyasema hayo huko ofisini kwake mazizini wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya udhalilishaji wa matamshi  kwa Allah (S.W)pamoja na Mtume wake yaliotolewa na Abdallah Saleh.

Sambamba na hayo ametoa onyo kwa waumini wa dini ya kiislam kutotamka maeno kama hayo kwa kuendekeza nafsi zao na kufikia kumtusi Mtume Muhammad(S.A.W) na kutoka kwenye twaa ya Mwenyezimungu (S.W) kwani kufanya hivyo kunapelekea kupata laana za Allah na Mtume wake.

Nae Naibu katibu Mufti wa Zanzibar Sheh Salum Fadhil Suraga amewataka maimamu wa miskiti ya Ijumaa kulaani matamshi yaliotolewa na kijana huyo ambae kwasasa amesha kamatwa na jeshi la Polisi na hatua za kisheri zinaendelea pamoja na kutopewa dhamana kituoni hapo juu ya tuhuma za udhalilishaji kwa Allah na Mtume wake .

chanzo: Zanzibar24.

Comments