Uchunguzi uliofanywa na Mwanahabari wetu umegundua kuwa wafanyabiashara hao marufu mapapazi wanavibali vya kufanya biashara katika maeneo hayo waliodai wamepewa na ofisi za halmashauri.
Akizungumza na Zanzibar24 mmoja wa wafanyabiashara hao amesema wanafanya biashara katika maeneo hayo baada ya kuruhusiwa na kupewa kibila kinachomruhusu kufanya biashara katika maeneo hayo.
Akizungumza juu ya tatizo hilo Mkurugenzi wa masoko kutoka kamisheni ya utalii Zanzibar Miraj Ukuti Ussi amesema serikali inawashajihisha wananchi kuzitumia fursa za utalii kufanya biashara katika maeneo yanayokubalika kisheria.
Amesema kufanya biashara kwenye fukwe ni kinyume cha sheria zinazoongoza sekta ya utalii kutokana na kuleta kero kwa watalii wanaofika kwenye hoteli kwa kupumzika.
chanzo;zanzibar24
Comments