OFISA
Mdhamin Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Pemba, Sihaba Haji Vuai,
amewataka maofisa wa Wilaya Kisiwani Pemba, kufanyakazi kwa kufuata ratiba
zinazotambulika kisheria, ili kurahisisha utendaji wa shughuli zao.
Ameyasema
hayo katika mkutano na maofisa hao, huko Chamanangwe, Wilaya ya Wete wakati
alipokuwa akiwaelekeza utaratibu wa utendaji kazi kwa watumishi wa umma.
Amesema
kuwa, watumishi wa umma ni lazima watekeleze shuguli zao kwa utaratibu maalum
unaotambulika na wanajamii anaowatumikia jambo ambalo litasaidia kwa kiasi
kikubwa kuondoa matatizo yanayoweza kujitokeza.
SaAidha
amewataka watumishi hao, kutoa taarifa kwa wakati zinapotokezea zarura za
kutofika katika eneo la kazi, ili kusaidia urahisi wa upatikanaji wa huduma na
taarifa.
Hata
hivyo amewasisitiza, watumishi hao, kufanya kazi kwa ushirikiano wa pamoja na
sekta nyengine za Serikali jambo ambalo litasaidia kupata mafanikio katika kazi
zao, huku akiwaahidi kuyafanyia kazi matatizo yanayorejesha nyuma juhudi zao
hatua kwa hatua kila hali itakaporuhusu.
Wakichangia
katika mkutano huo, maofisa hao, walisema kuwa, sambamba na ufuataji wa ratiba
wamekuwa wakikwazwa na usafiri wa kufikia katikamaeneo kwa wakati unaohitajika.
Kwa
upande wake, Ofisa Mifugo Wilaya ya Mkoani,
Abdalla Hamad Khamis, amesema kuwa ni vigumu kufuata ratiba katika utekeleaji
wa shughuli za mifugo kutokana na muingilianao wa matukio katika maeneo
tofauti.
Kwa
upande wake, Ofisa Uvuvi Wilaya ya Micheweni, Mzume Juma Faki, amewataka
maofisa wenzake kuongeza bidii ya kazi kwa kushirikiana katika utekelezaji wa
shughuli zao, ili kwenda samba na maagizo ya utumishi kwa umma.
Nae
Ofisa Mkuu wa Uendeshaji na Utumishi, Issa Nassor Bakar, amewaasa watumishi hao
kuwatumikia wanajamii kwa moyo mmoja kwa kufuta taratibu na kanuni za kisheria,
ili kufukia malengo yaliokusudiwa.
Comments