Katika nafasi yake ya Mjumbe Maalum wa Kamisheni hiyo, Rais Mstaafu
amemkabidhi Rais Hage Geingob Ripoti ya Kamisheni hiyo yenye mapendekezo
ya namna Dunia inavyoweza kukabili janga la Elimu kwa kuwekeza katika
Mpango wa Kizazi cha Elimu (A Learning Generation).
Mpango huo unalenga kuleta mapinduzi makubwa ya Elimu katika nchi
zinazoendelea ndani ya Kizazi Kimoja (miaka 30). Azma kuu ya Mpango huo
ni kuwezesha ifikapo mwaka 2040, watoto wote kote duniani wawe wanapata
elimu iliyo sawa, na kwa kiwango cha ubora unaolingana dunia nzima.
CHANZO: zanzibar24.
Comments