DPP aliyasema hayo ukingoni mwa mkutano wa wadau wa kujadili masuala
ya haki jinai uliowashirikisha watendaji wa vyombo vya sheria wakiwemo
polisi ,mawakili na waendesha mashtaka wakati akifunga mkutano huo.
Amesema kwa muda mrefu dhana ya rushwa na malalamiko ya wananchi
yamekuwa yakielekezwa kwa watendaji hao hivyo sio busara kukaa kimya na
kufumbia macho suala hilo kwani linaivunjia heshima taasisi hiyo.
Dpp huyo amesisitiza kwa taassisi nyengine kusimamia mambo matatu ili
kumaliza vitendo vya udhalilishaji na kesi za jinai nchini aliyoyataja
kuwa ni uwajibikaji, ushirikiano wa kitaasisi katika kufanya kazi na
kuepuka rushwa kwa watendaji.
chanzo:zanzibar24.
Comments