Diwani Omar aboresha zahanati katika kata yake, apeleka vitanda na kupanua maabara.

vitandaIkiwa imepita mwaka mmoja tangu Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Vingunguti, Omary Kumbilamoto ametekeleza nusu na robo ya ahadi zake katika kata yake kwa upande wa nafasi yake ya udiwani.

Wakati akielekea kuumaliza mwaka mmoja tangu aingie madarakani, amesema amekuwa akitumia juhudi zake binafsi pasipo kusubiri ruzuku kutoka serikalini kutekeleza ahadi zake.

Kumbilamoto ameyazungumza hayo ofisini kwake Jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii, ambapo amesema yeye kama Diwani aliona ni vema atumie juhudi zake akishirikiana na wadau kutoka katika kata yake kutekeleza jukumu lake kwani akisubiri ruzuku angechelewa.

Ameeleza badhi ya mafanikio kwa upande wa sekta ya afya aliyoyawezesha katika kata yake kuwa ni, kupunguza kilio cha kina mama kwa kupeleka vitanda vya kujifungulia katika Zahanati ya vingunguti.

Ili kuepukana na tatizo la giza katika Zahanati hiyo, amepeleka genereta moja, feni nne, na televisheni moja kwa ajili ya kupata habari mbalimbali.

Kumbilamoto pia amesema amefanikisha ununuzi wa magari mawili ya kubebea wagojwa kitu ambacho kilikua kero ya muda mrefu na kupelekea baadhi ya wagojwa kupoteza maisha kwa ukosefu wa usafiri.

Katika kuhakikisha suala la usafi katika wodi ya wazazi, amewajengea choo cha ndani katika wodi hiyo pamoja na mashine moja ya kufulia nguo za wagojwa.
Pia, amesema ndani ya mwaka huu amepeleka mashine ya kupimia presha, kisukari pamoja na tochi ya kupimia ugonjwa wa tons (mafindofindo) mapanzia ya kufunikia wagojwa wakizidiwa ama kufariki.

Aidha, amesema amefanikisha upanuzi wa maabara ya Zahanati hiyo.
 
“Kwa upande wa sekta ya afya hayo ndio mazuri na makubwa niliyoyafanya na kama ambavyo niliahidi kwa wananchi wangu kwamba nikiingia nitatatua kero zote za upande wa afya,” amesema Kumbilamoto.

Hata hivyo, anasema kwa upande wa elimu ukiacha misaada kutoka serikalini, aliyoyafanya yeye makubwa, ni kupeleka mashine moja ya kuzalishia nyaraka (printer) katika shule ya sekondari vingunguti ikiwa pamoja na kulipa deni la umeme 500,000 ambalo lilipelekea shule hiyo kukosa umeme mwaka mzima.

Bila kusahau ahadi zake kwa vijana Diwani huyo ametekeleza moja ya ahadi zake kwa kuwapatia jezi seti 14 katika vikundi vya timu za mpira na vikundi vya mazoezi ya asubuhi (joging clubs) katika kata yake.

Katika utekelezaji wa shughuli za kijamii Diwani Kumbilamoto amesema, amefanikiwa kufufua vyoo viwili vya umma ambavyo vipo nje ya machinjio na relini.

“Haya ni nusu na robo kati ya mambo ambayo niliahidi binafsi kuyatekeleza, kwa mwaka huu nimeyafanya hayo, naamini miaka ijayo nitafanya zaidi ya haya kwa ushirikiano wa wananchi wangu,” amesema.

chanzo; zanzibar24.

Comments