Bodi ya haki miliki yatakiwa kulinda haki za wasanii na wabunifu Zanzibar.

Bodi ya haki miliki Zanzibar imetakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na taratibu za kazi zao ili kulinda haki za wasanii na wabunifu Nchini.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Nne ya haki miliki huko mazizini, Waziri wa Katiba ,Sheria,Utumishi wa umma na utawala bora Mwalimu Haroun Ali Suleiman amesema wasanii wanafanya kazi kubwa ikiwemo kuelimisha jamii hivyo si vyema kukosa haki zao za msingi ikiwemo ulipwaji wa mirabaha.

Akizungumzia matatizo yanayoikabili Bodi hiyo Mwenyekiti wa bodi ya tatu Maryam Muhammed hamdani amesema wamekabiliwa na upungufu wa wafanya kazi katika bodi jambo ambalo linasababisha kushindwa kufanya kazi ipasavyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi Iddi Suleiman Suweid amesema kazi za haki miliki zinachangia kwa kiasi kikubwa katika kuleta maendeleo yanayotokana na kazi za wasanii na wabunifu na kutoa wito kwa wabunifu na wasanii kusajili.

chanzo; zanzibar24.

Comments