Alisema mpango huo ambao licha ya kuimarisha uhusiano wa muda mrefu uliopo kati ya Zanzibar na Cuba tokea Uhuru wa Mataifa hayo Mawili lakini pia utaongeza ushirikiano wa pande hizo zinazofanana katika Historia zake.
Balozi Seif Ali Iddi alitoa kauli hiyo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar wakati wa mazungumzo yake na Balozi wa Jamuhuri ya Cuba Nchini Tanzania Bwana Jorge Luis Lopez aliyefika kumuaga rasmi baada ya kumaliza muda wake wa kazi hapa Nchini.
Alieleza kwamba Cuba imekuwa mshirika mkubwa wa harakati za maendeleo ya Wananchi wa Zanzibar hasa katika kusaidia Taaluma ya Sekta za Afya na Kilimo chini ya Muasisi wa Taifa hilo Marehemu Fidel Castro.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alimuomba Balozi Jorge Luis licha ya kumaliza muda wake wa Kidiplomasia hapa Tanzania lakini bado ana nafasi ya kuisaidia Tanzania na Zanzibar kwa ujumla katika kuzitangaza Kiutalii kwa wawekezaji wa Nchi yake wakati atakaporejea nyumbani.
Aliishukuru Serikali ya Cuba kwa juhudi kubwa iliyochukuwa katika kusaidia maendeleo ya Wananchi wa Zanzibar ambao katika maisha yao yote ya baadaye wataendelea kuzikumbuka juhudi hizo.
Balozi Seif alifahamisha kwamba wataalamu wengi wa Cuba hasa wale wa Sekta ya Afya waliowahi kutoa Taaluma kwa vijana na Wananchi tofauti wa Zanzibar ni mfano halisi wa juhudi hizo.
Mapema Balozi wa Jamuhuri ya Cuba Nchini Tanzania Bwana Jorge Luis Lopez alisema kwamba uhusiano wa Kihistoria uliopo kati ya Zanzibar na Cuba utaendelea kama kawaida licha ya mabadiliko ya watendaji wanaosimamia uhusiano huo.
Balozi Lopez alimuhakikishia Balozi Seif kuwa mrithi wa kuchukuwa nafasi yake anayetarajiwa kuingia Nchini Tanzania wakati wowote kuanzia sasa ni Mwanadiplomasia mzoefu mwenye upeo wa kuzifahamu Siasa na mazingira ya Mataifa ya Bara la Afrika.
Bwana Lopez alimuahidi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba wazo lake la kumuomba kuitangaza Zanzibar atakaporejea nyumbani kwake atalifanyia kazi ipasavyo ili kuweka kumbu kumbu nzuri wa uwepo wake wa kazi Nchini Tanzania.
chanzo;zanzibar24.
Comments