Akizungumza na waandishi wa habari Huko katika ukumbi wa Wizara ya
Afya Mnazi Mmmoja Zanzibar mwenyekiti wa bodi hiyo amesema bodi
umesikitishwa kwa kiasi kikubwa na kosa alilolifanya Dk.Abllah Saleh
ambalo limewapa wasiwasi mkubwa viongozi wa dini,wananchi na viongozi wa
serikali katika maisha yao.
Hata hivyo amesema katika kipindi hicho cha kumsimamisha kazi
Dk.Abdallah taratibu za uchunguzi wa kosa lake zinaendelea kufanywa na
Bodi ya madaktari ili waweze kumchukulia hatua za kisheria
zinazostahiki.
Dk.Abdallah aliekuwa Daktari wa kitango cha wazazi aliwahi kufanya
kazi Katika hospitali ya mnazi mmoja Zanzibar pamoja na hospitali ya
wete Pemba na aliwahi kusoma masomo yake ya udaktari nchini Romania.
chanzo; zanzibar24.
Comments