Wizara ya Elimu Zanzibar imewataka wasimamizi wa mitihani kujiepusha kushiriki udanganyifu katika mitihani.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Riziki Pembe JumaWizara ya elimu Zanzibar imewataka Wasimamzi wa mitihani kuachana na tabia ya kushiriki udanganyifu katika vyumba vya mitihani ya wanafunzi ili kuimarisha sekta ya Elimu Nchini.

Akizungumza na waandishi wa Habari huko ofisini kwake mazizini Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Riziki Pembe Juma amesema kumekuwa na tabia kwa baadhi ya wanafunzi na wasimamizi wa mitihani  kufanya udanganyifu jambo ambalo linawathiri kitaaluma watahiniwa.

Aidha amesema katika kuondowa tatizo la udanganyifu wakati wa mitihani kila mwanafunzi anawajibu wa kutumia vizuri elimu waliopatiwa darasani ili kujiepusha na matatizo yasiyo ya lazima ikiwemo kufutiwa mitahani yao.

Akizungumzia suala la kuwepo kwa kambi za masomo ya ziada wakati wa usiku katika mazingira ya skuli ametowa wito kwa walimu wakuu wa skuli Binafsi na za Serikali kufunga kambi hizo wakati wote wa mitihani ili kuondoa  uwezekano wa udanganyifu linalofanywa na baadhi ya wanafunzi.

Jumla ya wanafunzi 30,950 wa darasa la sita, na Wanafunzi 24,907 wa kidatu cha pili  pamoja na Wanafunzi 35,597 wa darasa la nne wanatarajiwa kufanya mitihani ya taifa kuanzia Novembar 21,2016.

chanzo; Zanzibar24.

Comments