Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia zaanza rasmin.

wasichanaZaidi ya wasichana elfu saba wa shule za msingi na sekondari mkoani Mwanza wamekatisha masomo katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita kutokana na sababu mbalimbali  ikiwa ni pamoja na  mimba za utotoni.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa shirika la kutetea haki za wanawake la KIVULINI Yasini Ally wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.

Ametoa wito kwa jamii kuunganisha nguvu za pamoja ili kukomesha tatizo la mimba za utotoni.
Kauli mbiu ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ni funguka,pinga ukatili wa kijinsia,elimu salama kwa wote.

 chanzo;zanzibar24.

Comments