Serikali ya shauriwa kuwashajihisha wasimamizi wa Vituo vya kulelea watoto kuwapokea watoto wanaoishi na HIV.
Akizungumza na Zanzibar24 huko ofisini kwakwe Uwelezo Katibu wa
Jumuiya ya Watu wanaoishi na Ukimwi ZAPHA+ Consolata Jonh amesema
kumekuwa na wimbi kubwa la watoto wenye HIV wanaokosa huduma katika
familia zao na kukimbilia katika Jumuiya hiyo jambo linalopelekea kukosa
huduma za kutosha.
Aidha amesema mbali na mwamko mkubwa kwa jamii kupeleka watoto wao
kujiunga na Jumuiya lakini wamekuwa wakirejeshwa na baadhi ya vituo vya
kulelea watoto kutokubali kuwapokea na kuwasaidia watoto hao na
kupelekea kuwakosesha huduma muhimu wanzopatiwa watoto wenzao ikiwemo
elimu,mavazi na lishe ya uhakika.
Hata hivyo ametowa wito kwa wazazi na walezi kuwa mstari wambele
katika kuwatunza watoto wanaoishi na maambukizi ya HIV na kuachana na
tabia ya unyanyasaji ili waweze kunufaika na miradi ya kijamii ya
kuimarisha maendeleo.
Zaidi ya wananchama elfu tatu wanaoisha na HIV wamejunga na jumuiya
ya ZAPHA+ katika matawi 10 ya Unguja na Pemba kwa lengo la kutatuliwa
matatizo mbalibali yanayowakabili.
chanzo;Zanzibar24.
Comments