Akijibu swali katika kikao cha Baraza la Wawakilishi huko Chukwani
Naibu Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Lulu Msham amesema
katika mwaka wa Fedha 2015/16 wizara ya kilimo inaendelea na mkakati
wake wa kuotesha mikarafuu na kuigawa kwa wakulima ili waweze kuzalisha
kwa wingi zao hilo.
Aidha amesema kutokana na karafuu kuwa zao muhimu hapa Zanzibar
wakulima wanajukumu la kutunza miti ya mikarafuu ili waweze kuzalisha
zao hilo linaloendana na mahitaji ya soko.
Akizungumzia suala la kufa kwa miti ya mikarafuu Mashambani amesema
tatizo hilo linatokana na wakulima kupanda miche ambayo haiyaijakomaa
kupandwa mashambani pamoja uharibifu unaofanya na baadhi wa wafugaji
kufunga wanyama wao katika mashamba ya mikarafuu.
Kwa mujibu wa tathmini iliyofanywa na wizara ya kilimo na Maliasili,
mifugo na uvuvi zaidi ya Miche 326063 imeoteshwa na kutolewa kwa
wakulima wa zao hilo katika visiwa vya Unguja na Pemba.
chanzo;Zanzibar24
Comments