Baraza la Vijana la wilaya ya magharib A Unguja limeiomba Serikali kuwatafutia soko la kuuzia bidhaa za amali.
Akizungumza katika Uzinduzi wa Baraza hilo Mwenyekiti wa baraza la
Vijana wa Wilaya ya magharib A Farida Juma Hajji amesema wimbi kubwa la
vijana wameitikia wito wa serikali juu ya kujiaji na kujiunga na vyuo
vya amali lakini wanarejeshwa nyuma kwa kushindwa kuuza bidhaa
wanazozalisha.
Aidha ametowa wito kwa Serikali kuwatafutia utaratibu wa Upatikana
kwa elimu ya kuendesha Mabaraza ya Vijana na Biashara wanazozalisha kwa
wadau wa Maendelo ili waweze kuondokana na tatizo la ajira pamoja na
kujiepusha na kujiingiza katika vikundi hatarishi ikiwemo uvutaji wa
madawa ya klulevya.
Akizundua Baraza hilo Waziri wa nchi ofisi ya makamo wa Raisi
Muungano na Mazingira Januar Yussuf Makamba amesema serikali inatambua
uwepo wa matatizo mbalimbali yanayowakuba vijana na kuwataka kutovunjika
moyo katika shughuli za maendelo.
Aidha amesema pindipo vijana watajumuika pamoja katika kuanzisha
miradi ya maendeleo inayotokana na bidhaa wanazozalisha itawasaidia kwa
kiasi.
Nae Mkuu wa Wilaya ya Magharib A Mwinyi Ussi
Hassan ametowa wito kwa vijana hao kuendeleza utamaduni wa Mzanzibar
katika utekelezaji wa majukumu yao na kuachana na tabia ya kuiga vitendo
viovu ili kulinda utamaduni huo na kuleta maendeleo yanyoendana na Nchi
yao.
Zaidi ya Vijana mia tano wamejiunga na baraza hilo ili waweze
kujikwamua na tatizo la ajira linalowakabili na kupunguza kasi ya
ongezeko la umaskini Nchini.
chanzo; Zanzibar24
Comments