Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo , Maliasili , Mifugo na Uvuvi Zanzibar
Mh Juma Ali Juma amewataka wamiliki wa mahotel za kitalii na
wafanyabiashara wengine kisiwani pemba kununua mayai yanayozalishwa na
wafugaji kisiwani humo.
Amesema mayai yanayozalishwa na wafugaji kisiwani pemba ni yenye
viwango vinavyohitajika hivyo sivyema wakanunua mayai kutoka nje ya
pemba.
Kauli hiyo ameitowa wakati wa ziara ya kuwatembelea wafugaji wa kuku
katika shehia ya ziwani wilaya ya chake na kuona hali ya mrundikano
wa mayai kwa wingi yaliokosa soko kwa wafugaji hao.
Amesema wizara itaandaa utaratibu maalum ili kuhakikisha mayai
kutoka nje ya pemba wanayazuia ili wafugaji kisiwani pemba waweze kupata
soko lao la ndani.
Aidha katibu mkuu amewataka wafugaji hao wa kuku kutovunjika moyo
bali waendelee na kazi ya kuzalisha mayai kwa wingi kwani Serikali
inathamini juhudi na mchango wao katika mapambano dhidi ya adui maskini.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake Salama Mbarouk Khatib kwa niaba
ya wenzake amesema kwamba Serikali za Wilaya zitahakikisha
zinashirikiana na Wizara hiyo ili kuona kwamba mayai yote
yanayozalishwa na wafugaji kisiwani pemba yanauzwa.
Mmoja wa wafugaji Soud Ali Said akizungumza kwa niaba ya wafugaji
wenzake alimwambia Katibu mkuu kuwa ukosefu wa soko umepelekea pia
mifugo yao kuathirika na maradhi na njaa kutokana na wafugaja kukosa
fedha za kununulia mahitaji hayo .
Hata hivyo katika ziara hiyo zaidi ya trea mia tisa za mayai
zimeweza kununuliwa na wizara ya kilimo Maliasili ,Mifugo na Uvuvi
zanzibar kwa lengo la kuasaidia wafugaji hao.
chanzo;zanzibar24.co.tz
Comments