Watumishi wa umma na utawala bora wakatikwa kwenda wilayani na mikoani badala ya ofisi za mjini.

Na Hamad Shapandu.

Ofisa mdhamini ofisi ya Rais katiba sheria utumishi wa umma an utawala bora Masoud Ali Mohd ametoa wito kwa wafanya kazi wa wizara hiyo kujenaga tabia ya ushirikiano miongoni mwao kwa kua na kauli moja ya kiutendaji na kuacha tabia ya kufanya kazi kwa mazowea.

Amesema maadili yameporomoka katika sehema nyingi  za kazi kutokana na mashirikiano mabovu yasio fungamana na tabia ya wafanyakazi, huku  wakuu kufanya kazi katika wilaya na mikio ambako kero nyingi ziko huko na kushindwa kushughulikiwa kutokana na tabia zao za kubakia katika ofisi za mjini jambo ambalo limepitikiwa na wakati.

Nd. Mohd meyasema hayo huko ofisini kwake chake chake alipokua akizungumza na wakuu wa maidara na taasisi zilizo chini  ya wizara hiyo na kuwataka kuzingatia sheria  na kanuni za kazi kwa kuwa waadilifu  wakweli pamoja na kutoa huduma kwa jamii kwa kuzingatia haki , sheria, wajibu na mipaka ya wafanya kazi.

Aidha amewaonya wafanya kazi hao kuacha tabia ya kutumia fedha za umma kiholela na mfanya kazi yeyote atakae shindwa kufuata maadili sheria na taratibu za kazi, hatofumbuwa macho na kusema kua huu niwakati muafaka kwa wafanya kazi wenye tabia za aina hiyo, kujirekebisha kwani wazira yake imo mbioni kuzitafutia ufumbuzi changamoto zote zinazo wakabili.

Mratib wa idara ya rasilimali watu Bi Fat-hiya Mussa ametoa wito kwa mawizara, mashirika ya umma na taasisi binafsi kutumia fursa za kielimu wanazotoa kwa wafanya kazi wao wanaokwenda masomoni, kuchagua vyuo vinavyo tambulika na fani  zinazolingana na kazi zao ili kuepuka migogoro ya maslah inayo ikumba wizara nyingi kisiwani Pemba.


Nae mkurungenzi wa mashtaka Pemba Ali Rajabu Ali amesema kuwa changamoto kubwa iliyopo kisiwani Pemba ni wananchi waliowengi kutoifahamu ofisi hiyo inafanya kazi gani na kuwa ipo haja ya elimu kutolewa zaidi kuelimisha wananchi umuhimu wa uwepo wa ofisi hiyo, katika kusimamia utawala wa sheria na haki za binaadamu.

Comments