WAKAZI wa Wilaya ya Pangani mkoani Tanga wamemshukuru Rais John
Magufuli kwa kutimiza haraka ahadi yake ya kuwapatia kivuko kipya cha Mv
Tanga, kinachounganisha mji huo wa kihistoria na maeneo mengine
yaliyoko ng’ambo ya Mto Pangani.
Walibainisha hayo walipozungumza jana kwa nyakati tofauti katika
mahojiano wakati kivuko hicho kilichojengwa na Kampuni ya Songoro Marine
Transport Limited ya Dar es Salaam, kilipowasili mjini humo na kupokewa
na wananchi pamoja na baadhi ya viongozi wa Wakala wa Huduma za Ufundi
na Umeme nchini (Temesa).
Ali Mtoto mkazi wa Bweni alisema ana furaha kubwa kwa kivuko hicho
kuwasili kwa sababu kitawapunguzia adha na usumbufu walioupata kwa muda
mrefu walipolazimika kutegemea kivuko kimoja cha Mv Pangani II.
Naye Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Huduma za Ufundi na Umeme Wizara
ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Le-Kujan Manase alisema baada ya
kukipokea kutoka kwa mkandarasi na kufanyiwa majaribio wameridhika
kwamba kipo vizuri tayari kwa ajili ya kuhudumia wananchi.
Manase alisema katika ujenzi wa kivuko hicho cha Mv Tanga, serikali
imegharamia dola za Marekani 1, 869,000 hadi kukamilisha ujenzi huo. Kwa
upande wake, Mkurugenzi wa kampuni ya ujenzi wa kivuko hicho, Salehe
Songoro aliishukuru serikali kwa kuiamini kampuni hiyo hadi kuipatia
kazi hiyo.
chanzo;habarileo.
Comments