
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein
ameondoka leo kwenda nchini Uingereza kwa ziara maalum ya wiki mbili.
Katika
uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Dk. Shein, ambaye
amefuatana na mke wake Mama Mwanamwema, aliagwa na viongozi mbalimbali
wa Serikali wakiwemo mawaziri, Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza
la Mapinduzi, Makatibu Wakuu na viongozi wa vyombo vya ulinzi na
usalama.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi anatarajiwa kurejea nchini mara baada ya kumalizika ziara hiyo.
chanzo;zanzinews
Comments