Madiwa Kaskazini Pemba watakiwa kuto wabagua wanachi.

Madiwani wa wadi kumi zinazounda baraza la mji Wete Mkoa Wa Kaskazini Pemba  wametakiwa kutekeleza majukumu yao ya kazi kwa kuwatumikia wananchi wote bila ya kuwabagua kwa misingi ya vyama vyao .

Akizungumza katika hafla ya kuwaapisha madiwani , Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mhe Omar Khamis Othman amewataka kutekeleza majukumu kwa mujibu wa sheria  za tawala za mikoa namba 4 /2014.

Katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na katibu tawala mkoa huo Ndg Yussuf Mohammed Ali amewasisitiza madiwani hao kutobweteka na ushindi pamoja na dhamana mpya , bali wajipange kusimamia kazi kwa kushirikiana nawatendaji wa  baraza la mji .

Mapema mkurugenzi wa baraza la mji Wete Ndg Mgeni Othman Juma  amewataka madiwani hao kuwa waadilifu katika kusimamia mapato ya baraza ili fedha zinazokusanywa ziweze kutumika katika miradi ya maendeleo ya wananchi .

Nao madiwani wameahidi kutekeleza kwa vitendo ahadi walizozitoa wakati wa kampeni na kuwataka wananchi kuwapa ushirikiano ili kufanikisha majukumu yao .

Comments