Alichosema Dkt. Shein siku ya wafanyakazi Pemba.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dr.Ali Mohamed Shein amewataka wafanyakazi kufanya kazi kwa bidii  kwani serikali inathamini  juhudi za wafanyakazi wa ngazi zote  kutokana  na  kila mmoja anahaki sawa kwa mujibu wa sheria za kazi nchini.


Akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani  huko  Wete kisiwani Pemba amesema Serikali inatambua matatizo yanayowakumba wafanyakazi katika sehemu mbalimbali  hali ambayo isipodhibitiwa mapema inaweza kupelekea uwajibikaji mdogo katika sehemu za kazi.

Rais Shein amesema  uchumi wa Zanzibar unakuwa siku hadi siku kutokana na juhudi za wafanyakazi wa sekta mbalimbali za serikali na binafsi na kuwataka wafanyakazi kutovunjika moyo badala yake kuzidisha ari na bidii ya uwajibikaji huku akiahidi kuongeza kiwango cha mshahara pindi hali ya uchumi ikizidi kuimarika.

Mapema Akisoma Risala  kwa niaba ya wafanyakazi Zanzibar  Katibu Mkuu wa chama cha wafanyakazi Zanzibar ZATUC  Mwinyi Mohammed ameiyomba serikali  kuhakikisha inasimamia maslahi ya wafanyakazi wa ngazi zote kwani bado wanakumbwa na matatizo mbalimbali ambayo yanawarudisha nyuma kimaendeleo hivyo nivyema serikali kutafuta mbinu katika kuyapatia ufumbuzi kwani nao wanamchango mkubwa katika kukuza na kuongeza kasi ya ukuwaji wa uchumi Zanzibar.

Katibu huyo amesema nidhamu katika kazi ndio msingi wa maendeleo na kuahidi kuwa wafanyakazi  watazidisha ari katika utendaji  wao katika sehemu za kazi.

Kwaupande wake Waziri wa kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto Maudline Castico amesema ili kufikia katika uchumi wa kati Zanzibar lazima Serikali iimarishe  mabadiliko ya teknolojia,elimu na ujuzi kwa vijana,hali na nguvu kazi ilivyo na upatikanaji wa ajira hususani kwa vijana  wa rika tofauti.

Amesema hali ya baadae ya ulimwengu itabadilika kutokana na kukuwa kwa  utandawazi hivyo nivyema serikali kwa kushirikiana na wananchi kuanza kupanga mikakati itayosaidia katika kukabiliana na hali hyo.

 Zanzibar24

Comments