Waliojifanya Mabondia wakumbana na mkono wa sheria.

jamii
Mahakama ya mwanzo Mwanakwerekwe imewandisha kizimbani watuhumiwa Ali Hamad Ali (26) mkaaziwa Mtoni kigomeni, Khamis Hamad Ali (28) mkaazi wa Mtoni kigomeni na Salama Ali Seif (48) mkaazi wa  Mtoni kidatu kwa kosa la shambulio la kuumiza mwili.

Imedaiwa Mahakamani hapo na muendesha mashtaka wa Serikali Ali Yusuf mbele ya hakimu ali Abrahmani kwamba siku ya tarehe 30/5/ 2016 majira ya saa 10 jioni huko mtoni kijundu wote kwa pamoja walimpiga ngumi na mateke Maua  Khamis Mahtubu na kumsababishia maumivu makali mwilini mwake jambo ambalo ni kosa kisheria.


Mara baada ya kusomewa shtaka lao watuhumiwa hao walikataa na kuimba mahakam iwape dhaman jambo ambalo lilikubakiwa mahakani hapo.

Baada ya kutimiza masharti ya dhamana watuhumiwa hao kesi yao iliahirisha na kupangwa kusikilizwa tena tarehe 27/4 mwaka huu.
chanzo: zanzibar24.

Comments